SANINU LAIZER MCHIMBAJI MDOGO WA MADINI ALIYEIBUKA NA KUWA BILLIONEA TANZANIA


Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila amesema kuwa leo wizara inamtabua mchimbaji mdogo wa madini ya Tanzanite, Saninniu Laizer kuwa bilionea baada ya kupata mawe makubwa mawili yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8.

Mchimbaji huyo amepata mawe hayo mawili ambapo moja lina kilo 9.2 ambalo thamani yake ni shilingi bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.

“Na utofauti wake ni kwamba mawe ya uzito huo hayajawahi kupatikana kwenye machimbo ya Tanzanite tangu machimbo yaanze na yamepatikana ndani ya ukuta wa Mirereni kwahiyo hii ni rekodi mpya ya kupata mawe yenye uzito huo,” amesema Prof. Msanjila.

Profesa Msanjila amesema kuwa sekta ya madini inauwezo wa kumfanya mtu kuwa bilionea kwa haraka, ameongeza kuwa kunahitaji kuwa uwekezaji wa dhati katika sekta hiyo.

1592987909310.png


====​
Serikali imenunua mawe hayo kutoka kwa mchimbaji huyo na yatawekwa katika makumbusho ya taifa
Share on Google Plus

About JE UNAFAHAMU

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Comments :

Post a Comment